Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba Jean Charles Ahoua amejiunga na CR Belouizdad ya Algeria.
Ahoua amesajiliwa na timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili na nusu. Belouizdad wamenunua mkataba wake wa miezi sita uliokuwa umesalia na Simba.
Belouizdad tayari wamemtambulisha kiungo huyo aliyekuwa mfungaji bora wa ligi kuu ya NBC 2024/25.






