Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amekiri mambo yameharibika katika kikosi chake ikiwa ni siku chache tu baada ya kutabiriwa angejiuzulu nafasi yake kama kocha wa timu hiyo wiki hii.
Man City ilipoteza kwa mabao 3-1 dhidi ya timu ya Norway, Bodo/Glimt, katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, Jumanne na kuendelea kushuka katika msimamo wa michuano hiyo.





