Klabu ya Singida Black Stars imekamilisha usajili wa beki wa kushoto Miraji Abdallah 'Zambo' kutoka klabu ya Dodoma Jiji.
Zambo ameitumikia Dodoma Jiji kwa miezi mitano akijiunga na timu hiyo katika dirisha lililopita kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Coastal Union.
Beki huyo pia alihusishwa kujiunga na Simba katika dirisha lililopita lakini mpango wa kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi ulikwama baada aliyekuwa kocha wa Simba wakati huo Fadlu Davids kugomea usajili wake akimtaka Anthony Mligo.
Singida BS inatajwa kuwa mbioni kuachana na walinzi wake wawili wa kushoto Gadiel Michael na Imoro Ibrahim nafasi zao zikichukuliwa na Zambo na Rahim Shomari.
Gadile huenda akapishana na Zambo akielekea Dodoma Jiji.



