TRA United imerejea kwa nguvu kubwa kwenye ligi kuu ya NBC baada ya mapumziko ya Afcon 2025 ikiichapa KMC mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.
Mabao ya Kassim Mgoya, Joseph Akandwanaho na Hance Mabena akijifunga, yametosha kuihakikishia TRA United alama tatu muhimu.
Unaweza kusema jahazi la KMC linazidi kuzama kwani watoza ushuru hao kutoka Kinondoni jijini Dar es salaam, wameendelea kujikita mkiani mwa msimamo wa ligi.




