Yanga yapoteza ugenini dhidi ya Al Ahly

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd January 2026


Yanga yapoteza ugenini dhidi ya Al Ahly

Mabao mawili ya Trezeguet yameihakikishia Al Ahly ushindi muhimu wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa ligi ya mabingwa uliopigwa uwanja wa Borg El Arab huko Misri.

Yanga ilicheza kwa nidhamu kubwa kipindi cha kwanza lakini walipoteza umakini dakika za lala salama kipindi cha kwanza Trezeguet akifunga bao la uongozi kwa kichwa.

Kipindi cha pili kocha wa Yanga Pedro Goncalves alifanya mabadiliko kidogo ya kimbinu akiwaingiza Mudathir Yahya na Pacome Zouzoua akijaribu kusaka bao la kusawazisha.

Hata hivyo kupotea kwa umakini eneo la kati ya uwanja kukawanufaisha tena Al Ahly kupitia shambulizi la kujibu lililowekwa kambani na Trezeguet kwa mara nyingine.

Yanga ilitengeneza nafasi nzuri zaidi kwenye kipindi cha kwanza lakini Maxi Nzengeli na Allan Okello walikosa kuifungia timu yao.

Yanga sasa inarejea Tanzania huku ikifahamu inapaswa kushinda mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki ijayo dimba la New Amaan Complex visiwani Zanzibar.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.