Simba imepoteza mchezo wa tatu mfululizo ligi ya mabingwa barani Afrika (CAFCL) ikikubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Esperance huko Tunisia.
Simba iliuanza mchezo huo kwa kasi mapema tu ilipoteza nafasi kupitia kwa Jonathan Sowah baada ya shuti lake ndani ya 18 kuokolewa na mlinda lango wa Esperance.
Bao pekee la Esprance lilifungwa na Jack Diarra akimzidi mbio mlinzi wa kulia wa Simba Shomari Kapombe na kuujaza mpira kimiani kiurahisi.
Simba ilitawala mchezo zaidi kwenye kipindi cha pili lakini hakukuwa na nafasi zilizotengenezwa safu ya ulinzi ya Esperance ikiondoa hatari zote langoni.
Sio matokeo mazuri kwa Simba kwani sasa italazimika kushinda mechi tatu zilizobaki mbili zikiwa nyumbani na moja ugenini.
Mchezo unaofuata ni dhidi ya Esperance ukitarajiwa kupigwa wiki ijayo dimba la Benjamin Mkapa.
Baada ya mchezo huo Simbaa itasalia na mechi mbili dhidi ya Petro Atletico (ugenini) na Stade Malien (nyumbani).