Aliyekuwa kocha wa Young Africans SC (Yanga) msimu uliopita, Miloud Hamdi, ametangaza kujiuzulu rasmi wadhifa wake wa ukocha katika klabu ya Ismaily SC ya Misri.
Hamdi ametangaza uamuzi huo jana, Jumatatu Januari 26, 2026, baada ya kuitumikia Ismaily kwa kipindi cha miezi sita pekee, tangu alipojiunga na klabu hiyo Julai 3, 2025, akitokea Yanga.
Katika ujumbe wake wa kuaga, Hamdi ameonyesha shukrani kwa uongozi, wachezaji na wafanyakazi wa klabu hiyo, akisisitiza mshikamano waliokuwa nao licha ya changamoto.
Aliyekuwa kocha wa Young Africans SC (Yanga) msimu uliopita, Miloud Hamdi, ametangaza kujiuzulu rasmi wadhifa wake wa ukocha katika klabu ya Ismaily SC ya Misri.
Hamdi ametangaza uamuzi huo jana, Jumatatu Januari 26, 2026, baada ya kuitumikia Ismaily kwa kipindi cha miezi sita pekee, tangu alipojiunga na klabu hiyo tarehe Julai 3, 2025, akitokea Yanga.
Katika ujumbe wake wa kuaga, Hamdi ameonyesha shukrani kwa uongozi, wachezaji na wafanyakazi wa klabu hiyo, akisisitiza mshikamano waliokuwa nao licha ya changamoto.
"Nawashukuru kwa nyakati tulizopita pamoja katika vipindi vigumu. Lakini tulifanikiwa kuwa tumeungana pamoja. Tulikuwa familia halisi na wataalam wa tiba na sekretarieti ya klabu ikiongozwa na Ahmed Salah,” amesema Hamdi.
“Kufuatia kujiuzulu kwangu klabuni, kipekee nitakumbuka nyakati nzuri pamoja na mashabiki wetu. Nawatakia kila la kheri.”
Ingawa kocha huyo hakutaja wazi sababu za kujiuzulu, wachambuzi wa soka wanaeleza kuwa matokeo yasiyoridhisha ya Ismaily chini ya uongozi wake yanaweza kuwa chanzo kikuu cha uamuzi huo.
Tangu Hamdi aanze kazi rasmi Julai mwaka jana, Ismaily imecheza jumla ya mechi 19 katika mashindano mbalimbali, ikifanikiwa kupata ushindi mara nne tu, sare mbili, huku ikipoteza mechi 13—rekodi iliyoiweka klabu hiyo katika presha kubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wa soka nchini Misri.



