International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Januari 28 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatano Januari 28 2026

Chelsea wanamwona kiungo mshambuliaji Cole Palmer, 23, kama mchezaji "asiyeguswa" licha ya kuhusishwa na Manchester United, na wanamchukulia mchezaji huyo wa England aliye na mkataba hadi 2033 kuwa mhimili mkubwa wa mustakabali wa klabu hiyo. (Sky Sports)

Brighton wamekataa ofa kutoka Nottingham Forest kwa ajili ya beki wake wa England mwenye umri wa miaka 34, Lewis Dunk. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa Chelsea Raheem Sterling anatarajiwa kuondoka kabla ya dirisha la usajili wa majira ya baridi kufungwa, huku pande zote zikifanya mazungumzo ya kufanikisha kuondoka kwa mchezaji huyo wa zamani wa England mwenye umri wa miaka 31. (Fabrizio Romano)

West Ham wanaangalia uwezekano wa kuwasajili kwa mkopo kipa wa Tottenham kutoka Czech, Antonin Kinsky, 22, na beki wa Chelsea kutoka Ufaransa, Axel Disasi, 27. Hata hivyo, ili ifanikiwe, Hammers watalazimika kumrejesha beki wa Brazil Igor Julio, 27, Brighton. (Guardian)

Wawakilishi wa kipa wa Manchester United mwenye umri wa miaka 29, Andre Onana, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Trabzonspor, wamefanya mazungumzo kuhusu kurejea kwa mlinda mlango huyo wa Cameroon katika klabu yake ya zamani Inter Milan majira ya kiangazi. (Mail)

Wolves wako kwenye mazungumzo ya kumsajili kwa mkopo kiungo wa England mwenye umri wa miaka 25, Angel Gomes, kutoka klabu ya Ufaransa Marseille. (Talksport)

Mshambuliaji wa Auxerre Lassine Sinayoko anasakwa na pia na Wolves, huku klabu za Championship, Coventry City na Middlesbrough nazo zikionesha nia ya kumsajili mchezaji huyo wa Mali mwenye umri wa miaka 26. (Football Insider)

Burnley wako kwenye mazungumzo na West Ham kuhusu kumsajili kwa mkopo kiungo wa England mwenye umri wa miaka 31, James Ward-Prowse. (Telegraph)

Sunderland wamepuuza taarifa zinazodai kuwa mshambuliaji wa Hispania mwenye umri wa miaka 20, Eliezer Mayenda, anaweza kuruhusiwa kuhamia Paris FC. (The I paper)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’