Jana Simba ilitambulisha usajili wa nyota mwingine aliyesajiliwa na Wekundu hao wa Msimbazi katika dirisha hili.
Mapema, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali alidokeza kuwa usajili huo umekamilishwa na mzabuni wa jezi kampuni ya JayRutty ikitimiza ahadi kwa Wanasimba.
Kiungo mshambuliaji Inno Jospin Loemba (21) kutoka klabu ya Colombe Sports ya Cameroon ndiye aliyesajiliwa na JayRutty
Baada ya utambulisho wake, Loemba anajiunga na kikosi cha Simba ambacho leo kitashuka uwanja wa Isamuhyo kuikabili Mashujaa Fc katika mchezo wa liigi kuu ya NBC.
Baada ya mchezo huo, Simba itaanza maandalizi ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Esperance utakaopigwa Jumapili, Februari 1.



