Ushindi wa bao 1-0 ambao Azam Fc waliupata dhidi ya Nairobi United jana umefufua matumaini ya wauza ice-cream hao katika kuisaka tiketi ya kufuzu robo fainali ya kombe la Shirikisho (CAFCC).
Bao la mapema lililofungwa na Feisal Salum 'Fei Toto' lilidumu kwa dakika zot 90 na kuishuhudia Azam Fc ikiipiga Nairobi United 'nje-ndani' sasa wakifikisha alama 6 kundi B huku Nairobi United wakipoteza matumaini.
Katika mchezo uliopigwa mapema, klabu ya Otoho dβOyo ya Jamhuri ya Congo ikaibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars ya Tanzania katika mchezo ambao mlinda lango wa Singida BS Metacha Mnata alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Tukio hilo la kadi nyekundu limekuwa mojawapo ya sababu kuu zinazotajwa kuchangia matokeo ya mchezo huo, huku Singida ikilazimika kupambana katika mazingira magumu kwa zaidi ya dakika 60.
Singida BS wako nafasi ya tatu kundi D wakiwa na alama 4 bado wako kwenye mbio za kuisaka robo fainali.