International,Normal News,Local, Yanga, Ahly

Al Ahly yapania mchezo dhidi ya AS FAR

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Feb 2026
Al Ahly yapania mchezo dhidi ya AS FAR

Mashabiki 45,900 wanatarajiwa kushuhudia mechi ya uamuzi ya Kundi B ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAFCL) kati ya Al Ahly na AS FAR.

Mchezo huo utachezwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Cairo, Misri, Jumapili, Februari 15, ambapo Al Ahly itakuwa mwenyeji.

Mamlaka za soka za Misri kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) zimetoa kibali cha idadi hiyo ya mashabiki kuhudhuria mchezo huo kwa kuzingatia sababu za kiusalama, kutokana na ukubwa na ushindani wa mechi hiyo.

Kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa, Al Ahly imetakiwa kutenga tiketi 2,200 kwa ajili ya mashabiki wa AS FAR wanaotarajiwa kusafiri kutoka Morocco hadi Misri kuisapoti timu yao katika pambano hilo.

Al Ahly tayari imejihakikishia tiketi ya kufuzu hatua ya robo fainali ya CAFCL. Hata hivyo, ushindi au sare katika mechi hiyo utaiwezesha kumaliza kinara wa msimamo wa Kundi B.

Kwa upande wa AS FAR, sare au ushindi utawahakikishia nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali.

Matokeo ya ushindi kwa Al Ahly ndio yanayobeba matumaini ya Yanga ya Tanzania kufuzu robo fainali kama itaibuka na ushindi kwenye mchezo dhidi ya AS FAR.

Yanga itahitaji kuibuka na ushindi wa kuanzia mabao 2-0 ili kunufaika na matokeo ya ushindi kwa Al Ahly.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’