International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa Februari 13 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Feb 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Ijumaa Februari 13 2026

Paris Saint-Germain wako tayari kushindana na vilabu vya Ligi Kuu England kama Chelsea, Manchester United na Tottenham kwa kutoa ofa ya pauni milioni 100 kwa kiungo wa Cameroon mwenye miaka 22, Carlos Baleba, kutoka Brighton & Hove Albion. (Fichajes)

Tottenham Hotspur wameonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji Mmrekani aliyewahi kuichezea Chelsea, Christian Pulisic (27), ambaye yuko tayari kurejea England akitokea AC Milan msimu huu wa joto. (Teamtalk)

Spurs wanatafuta kocha wa muda kabla ya kujaribu kumrejesha kocha wa Marekani, Mauricio Pochettino, baada ya Kombe la dunia baadaye mwaka huu. (Sun)

Manchester United wana matumaini makubwa kuwa beki wa England mwenye miaka 32, Harry Maguire, ataongeza mkataba wake Old Trafford zaidi ya mwisho wa msimu huu. (Teamtalk)

Kipaumbele cha Newcastle United katika dirisha la usajili wa majira ya joto ni kusajili mshambuliaji, huku klabu hiyo ikitazamia kumuuza Mjerumani mwenye miaka 23, Nick Woltemade, baada ya uhamisho wake wa rekodi ya klabu mwezi Agosti. (Football Insider)

Mshambuliaji wa Poland mwenye umri wa miaka 37, Robert Lewandowski, atasubiri kuamua hatma yake hadi baada ya uchaguzi wa urais wa klabu mwezi Machi, huku akiwa na ofa kutoka AC Milan, Atletico Madrid, Chicago Fire, Fenerbahce na vilabu vya Saudi Arabia. (Mundo Deportivo)

Bologna wamempa mkataba mpya wa miaka minne na nusu mshambuliaji wa Argentina mwenye miaka 21, Santiago Castro, huku Chelsea, Everton na Aston Villa zikiwa miongoni mwa vilabu vilivyokuwa vinamfuatilia. (Football Italia)

Manchester United, Arsenal, Chelsea na Tottenham ni miongoni mwa vilabu vya Ligi Kuu vinavyomfuatilia kwa karibu kiungo wa Serbia mwenye miaka 20, Aleksandar Stankovic, wa Club Brugge. (Teamtalk)

Manchester United wanatarajiwa kutuma wawakilishi kumuangalia beki wa Ufaransa mwenye miaka 25, Pierre Kalulu, wa Juventus, katika mechi dhidi ya Inter Milan. (Tuttosport)

Manchester United pia wanamfuatilia beki wa Gambia mwenye miaka 19, Abubacarr Sedi Kinteh, wa Tromso, pamoja na beki wa kati wa Hispania mwenye miaka 18, Hugo Fernandez, kutoka Valencia. (Mail)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’