Shirika la Soka Barani Afrika (CAF) limekamilisha droo ya hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika (TotalEnergies CAF Confederation Cup 2025/26) leo Jumanne, Februari 17, 2026, jijini Cairo, Misri.
Katika hafla hiyo iliyofanywa katika makao makuu ya CAF, vilabu nane vilivyofanikiwa kutoka hatua ya makundi vimepangwa kukutana katika mechi za mtoano ambazo zitaamua nani wataendelea nusu fainali ya mashindano hayo.
Baada ya droo hiyo, ratiba ya mechi za robo fainali ya Kombe la Shirikisho imebainika kama ifuatavyo: Al Masry (Misri) atalazimiana na CR Belouizdad (Algeria), OC Safi (Morocco) atacheza dhidi ya Wydad AC (Morocco), AS Otohô (Congo) atakutana na Zamalek SC (Misri) na AS Maniema Union (Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo) atacheza na USM Alger (Algeria).
Mechi hizi zitachezwa kwa mfumo wa nyumbani na ugenini kama ilivyo desturi katika mashindano ya klabu barani Afrika.
Hii inaweka wazi safari ya timu hizo katika hatua za mtoano kuelekea fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu, huku mashabiki wa soka wakitarajia mechi za kusisimua kati ya vilabu vyenye historia na ushawishi katika soka la klabu Afrika.
Michuano ya robo fainali itaanza rasmi mwishoni mwa mwezi Machi, ambapo leg ya kwanza itapigwa kati ya Mach 13 na 15, 2026, na leg ya pili kati ya Mach 20 na 22, 2026. Washindi wa kila mfululizo watapangwa droo upya kuelekea hatua ya nusu fainali, kabla ya hatimaye kushindana katika mechi ya fainali ya mashindano hayo.



