Simba, Yanga, Azam Fc, Singida BS vitani Ligi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd February 2026


Simba, Yanga, Azam Fc, Singida BS vitani Ligi

Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo Jumapili ambapo mechi za viporo zinazohusisha timu zilizokuwa kwenye majukumu ya Kimataifa zitakuwa uwanjani.

Saa 8 mchana mchana Singida BS watakuwa ugenini mkoani Dodoma kuikabili Mtibwa Sugar.

Saa 10:15 jioni Azam Fc nao watakuwa ugenini kumenyana na KMC huku mabingwa watetezi Yanga wakitarajiwa kuumana na Namungo huko Ruangwa majira ya saa 1 usiku.

Saa 3 usiku mkoani Dodoma mchezo mwingine kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Simba utapigwa uwanja wa Jamhuri.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.