Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo Jumapili ambapo mechi za viporo zinazohusisha timu zilizokuwa kwenye majukumu ya Kimataifa zitakuwa uwanjani.
Saa 8 mchana mchana Singida BS watakuwa ugenini mkoani Dodoma kuikabili Mtibwa Sugar.
Saa 10:15 jioni Azam Fc nao watakuwa ugenini kumenyana na KMC huku mabingwa watetezi Yanga wakitarajiwa kuumana na Namungo huko Ruangwa majira ya saa 1 usiku.
Saa 3 usiku mkoani Dodoma mchezo mwingine kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Simba utapigwa uwanja wa Jamhuri.




