International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, Februari 23 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Feb 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumatatu, Februari 23 2026

Manchester City itakabiliana na pambano la kutaka kumbakisha kiungo wa kati wa Uhispania Rodri msimu huu, huku Real Madrid na Barcelona wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29. (Bild - In Germany)

Matumaini ya Liverpool kumsajili beki wa Roma Zeki Celik yameongezeka baada ya wakala wake kukataa uwezekano wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki mwenye umri wa miaka 29 kujiunga na Juventus. (Mirror)

Arsenal na Chelsea wanaisukuma Barcelona katika kumsaka mshambuliaji wa Atletico Madrid na Argentina Julian Alvarez, 26. (TeamTalks)

Juventus wamemtambua mlinda lango wa Tottenham mwenye umri wa miaka 29 Guglielmo Vicario kama shabaha kuu msimu huu, lakini watakabiliwa na ushindani kutoka kwa Inter Milan. (Gazzetta dello Sport - In Italy)

Newcastle itamuuza mshambuliaji wa Ujerumani Nick Woltemade msimu huu wa joto ikiwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 atataka kuondoka katika klabu hiyo. (Football Insider)

Arsenal wako mbele ya Manchester City na Newcastle katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Sporting raia wa Uhispania Ivan Fresneda, 21. (Fichajes - In Spanish)

Kuwasili kwa Fresneda kunaweza kumfanya beki wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28 Ben White kuondoka Arsenal. (TeamTalks)

Manchester United na Arsenal wanapewa nafasi kubwa ya kumsajili beki wa Eintracht Frankfurt, 22, Nathaniel Brown msimu huu wa joto. (Caughtoffside)

Chelsea inaweza kumruhusu mlinzi wa Uingereza Trevoh Chalobah, 26, kujiunga na Aston Villa msimu huu wa joto ikiwa The Blues wanaweza kusajili mbadala wake. (Football Insider)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
14m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’