Sowah matatani Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th February 2026


Sowah matatani Simba

Mshambuliaji wa Simba, Jonathan Sowah, hatakuwa sehemu ya kikosi kitakachoshuka dimbani Jumatano kuikabili Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC, licha ya kumaliza adhabu ya kukosa mechi tano.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kuwa uamuzi wa kumwondoa kwenye mpango wa mchezo huo umefanywa na kocha mkuu, Steve Barker, kufuatia matukio ya kujirudia ya utovu wa nidhamu.

Imeelezwa kuwa mshambuliaji huyo tayari amerejea jijini Dar es Salaam, huku suala lake likitarajiwa kuwasilishwa katika Kamati ya Nidhamu ya klabu kwa hatua zaidi. Endapo atapatikana na hatia, huenda akachukuliwa hatua kali zaidi, ikiwemo kusimamishwa.

Tangu alipoanza kuinoa Simba, Barker amekuwa akisisitiza umuhimu wa nidhamu, akieleza wazi kuwa kila mchezaji anapaswa kuzingatia maadili na taratibu za timu bila kujali hadhi yake kikosini.

Hii ni mara ya pili kwa Sowah kuingia matatani akikabiliwa na tuhuma hizo hizo za utovu wa nidhamu.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.