Droo ya hatua ya 16bora ya UEFA Champions League kwa msimu wa 2025/26 imefanyika leo Ijumaa, Februari 27, 2026, jijini Nyon, Uswisi, ikiwakutanisha vilabu 16 bora barani Ulaya.
Droo hiyo, yenye uzito mkubwa kwa mashabiki wa soka duniani, ilibainisha mechi zitakazochezwa mwanzoni Machi, zikilenga kuonyesha timu ambazo zitasonga mbele kuelekea robofainali na fainali iliyopangwa Mei 30, 2026, jijini Budapest, Hungary.
Katika droo iliyofanyika, Paris SaintGermain imepangwa kukutana na Chelsea, huku Galatasaray ikipangwa dhidi ya Liverpool.
Mmoja wa mechi zinazotarajiwa kwa mvuto mkubwa ni kati ya Real Madrid na Manchester City, mwendelezo wa pambano kubwa la vilabu vya Uropa ambalo limekuwa likirudiwa katika michuano ya mabingwa.
Atalanta imepangwa kukutana na Bayern Munich, ikiwa ni pambano lenye changamoto kubwa kwa pande zote mbili. Kwa upande mwingine, Newcastle United itacheza na Barcelona, wakati Atlético Madrid ilipangwa na Tottenham Hotspur. Pia, Bodø/Glimt itakutana na Sporting CP, na Bayer Leverkusen itaingia dimbani dhidi ya Arsenal.
Michezo ya hatua ya 16 bora utafanyika kwa viwango viwili – leg ya kwanza itachezwa kati ya Machi 10 na 11, 2026, na leg ya marudiano kati ya Machi 17 na 18, 2026. Baada ya hatua hii, timu zilizofanikiwa zitapambana katika robofainali, nusu fainali na hatimaye fainali itakayofanyika Mei 30, 2026 katika uwanja wa Puskás Arena, Budapest.




