Aliyekuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Almas Kasongo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa timu za taifa Tanzania.
Kasongo ambaye alisimamishwa mwaka jana, ametangazwa leo Jumamosi, Februari 28, 2026 katika Mkutano Mkuu wa TFF ambao umefanyika Kahama, Shinyanga.
Aidha Baraka Kizuguto ametangazwa kuwa Mkurugenzi wa mashindano huku Oscar Mirambo akiendelea Kukaimu nafasi ya Katibu Mkuu wa TFF.
Mkutano Mkuu wa 20 wa TFF umefanyika leo Kahama mkoani Shinyanga ukiongozwa na Rais wa TFF Wallace Karia.



