Baada ya watani wa jadi Yanga na Simba kumalizana jana katika mchezo uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar na kumalizika kwa suluhu ya bila kufungana, mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo kwa mechi nyingine mbili kupigwa.
Singida BS watakuwa wenyeji wa Coastal Union mchezo utakaopigwa uwanja wa Airtel huku Pamba Jiji wakiwakaribisha Azam Fc mchezo utakaopigwa uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Mechi zote zinatarajiwa kupigwa saa 10 jioni.




