Obasogie kuanza na Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th March 2026


Obasogie kuanza na Simba

Jana klabu ya Singida BS ilitangaza kumsamehe mlinda lango wake Amas Obasogie ambaye awali alifungiwa kwa tuhuma za upangaji wa matokeo.

Kupitia taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, Singida BS walitangaza kumsamehe baada ya kamati iliyofanya uchunguzi wa tuhuma zake kutobaini ushahidi wowote.

Obasogie amerejeshwa kikosini siku chache kabla ya Singida BS kuikabili Simba kwenye mchezo wa ligi kuu utakaopigwa March 11 uwanja wa Airtel huko Singida.

Anaungana na kiungo Khalid Aucho ambaye pia alisamehewa na klabu hiyo baada ya kuomba radhi. Aucho alisimamishwa kwa tuhuma za utovu wa nidhamu.

Nyota hao huenda wakawa sehemu ya kikosi kitakachoikabili Simba kwenye mchezo wa ligi kuu siku ya Jumatano.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.