Klabu ya Yanga imethibitisha kuwa nahodha wake msaidizi Dickson Job amefanyiwa upasuaji wa goti Afrika Kusini.
Job ambaye ni beki tegemeo wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars', alipata majeraha kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex mapema mwezi huu na kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.
Job alipata majeraha hayo baada ya kugongana na kiungo mshambuliaji wa Simba Inno Loemba na kulazimika kutoka nje nafasi yake ikichukuliwa na Bakari Mwamnyeto.
Job anatarajiwa kuwa nje kwa takribani wiki nane au zaidi kutegemeana na uponaji wa jeraha lake baada ya upasuaji huo uliofanikiwa.
Yanga itamkosa beki huyo katika kipindi muhimu ambacho wanakabiliwa na mechi mfululizo.



