Yanga yaichapa Prisons 1-0 Dodoma

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th March 2026


Yanga yaichapa Prisons 1-0 Dodoma

Yanga imeendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi ikiichapa Tanzania Prisons bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Mshambuliaji Laurindo Aurelio ndiye aliyepeleka kilio kwa maafande hao akifunga bao dakika ya 78 akimalizia mpira uliotemwa na mlinda lango Moussa Mbissa baada ya shuti la Allan Okello kupitia mpira w adhabu.

Depu aliingia kipindi cha pili na alihitaji takribani dakika 10 tu kuifungia Yanga bao hilo katika mchezo ambao mpango wa Prisons ulikuwa kulinda lango lao.

Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Yanga ikitawala lakini haikuwa rahisi kulipenya lango Prisons kabla ya bao la Depu.

Ni alama tatu zinazoifanya Yanga ifikishe alama 35 na hivyo kuendelea kujiweka juu ya msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama 7.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.