Real Madrid, Arsenal zapeta robo fainali, Man City, Chelsea zatupwa nje UEFA CL

Joel JJ By Joel JJ • 18th March 2026


Real Madrid, Arsenal zapeta robo fainali, Man City, Chelsea zatupwa nje UEFA CL

Michuano ya UEFA Champions League imeendelea kushika kasi barani Ulaya huku baadhi ya timu vigogo zikitinga hatua ya robo fainali baada ya mechi za mkondo wa pili wa hatua ya 16 bora zilizochezwa Jumanne, Machi 17, 2026.

Miongoni mwa matokeo makubwa ya usiku huo, Paris Saint-Germain iliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Chelsea FC, na kufuzu kwa jumla ya mabao 8-2. PSG walionyesha ubora mkubwa katika mchezo huo, wakitawala sehemu kubwa ya dakika 90.

Katika mechi nyingine iliyovuta hisia za mashabiki wengi, Real Madrid iliichapa Manchester City kwa mabao 2-1 ugenini, ushindi uliowapa tiketi ya robo fainali kwa jumla ya mabao 5-1. Nyota wa Madrid, Vinícius Júnior, alikuwa mhimili kwa kufunga mabao yote mawili.

Nayo Arsenal FC iliendeleza kiwango bora baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bayer Leverkusen, matokeo yaliyowawezesha kusonga mbele katika hatua inayofuata ya mashindano.

Kwa upande mwingine, mechi kati ya Sporting CP na Bodø/Glimt ilikuwa sehemu ya ratiba ya siku hiyo huku timu ya Bodø/Glimt wakiondoshwa michuanoni kwa kipigo cha mabao 5-0, Sporting wametinga robo fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-3

Ratiba ya Mechi za Leo

Michuano hiyo inaendelea leo Jumatano, Machi 18, 2026, kwa michezo mingine ya mkondo wa pili wa hatua ya 16 bora, ambapo vigogo kadhaa wanatarajiwa kushuka dimbani kuwania nafasi za robo fainali.

Miongoni mwa mechi zinazotarajiwa ni ile kati ya FC Barcelona dhidi ya Newcastle United, mchezo unaotarajiwa kuwa mkali kufuatia sare ya 1-1 katika mechi ya kwanza.

Aidha, Bayern Munich watakuwa na kibarua chepesi wanapokutana na Atalanta BC, baada ya ushindi mkubwa wa mabao 6-1 walioupata katika mchezo wa awali.

Katika michezo mingine, Liverpool FC watakuwa na kazi ngumu ya kusaka ushindi dhidi ya Galatasaray SK, huku Tottenham Hotspur wakikabiliana na Atlético Madrid katika pambano lingine lenye ushindani mkali.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.