Kocha Pep Guardiola anatarajiwa kufanya uamuzi muhimu kuhusu mustakabali wake ndani ya Manchester City baada ya kukamilika kwa fainali ya Carabao cup dhidi ya Arsenal itakayochezwa Jumapili.
Kwa mujibu wa taarifa, kocha huyo Mhispania ataondoka kwa mapumziko mafupi mara baada ya mchezo huo, ambapo atapata muda wa kutafakari na kufanya maamuzi kuhusu hatma yake. Uamuzi huo unatarajiwa kubainisha kama ataendelea kuinoa City katika msimu ujao au la, jambo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki pamoja na wadau wa soka duniani.
(Chanzo: MailSport)
Β