Tudor afutwa kazi Tottenham Hotspurs

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th March 2026


Tudor afutwa kazi Tottenham Hotspurs

Klabu ya Tottenham Hotspur imethibitisha rasmi kumfuta kazi kocha wake Mkuu Igor Tudor leo Jumapili, Machi 29, 2026, baada ya kipindi kifupi lakini chenye matokeo mabaya ndani ya timu.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu, imekubaliwa kwa pande zote kwamba Tudor ataondoka mara moja, ikiwa ni pamoja na baadhi ya makocha wenzake.

Kocha huyo raia wa Croatia alikaa madarakani kwa takriban siku 44 pekee na kuiongoza timu katika mechi saba tu, moja ya vipindi vifupi zaidi kwa kocha katika historia ya Premier League.

Sababu kuu ya kuondoka kwake ni mwenendo mbaya wa matokeo. Katika mechi zake saba:

  • Alipoteza mechi 5
  • Hakushinda hata mechi moja ya ligi
  • Timu ilibaki karibu na kushuka daraja (nafasi ya 17)

Kwa sasa Spurs walikuwa pointi moja tu juu ya eneo la kushuka daraja, hali iliyozua presha kubwa kutoka kwa mashabiki na uongozi wa klabu.

Ripoti zinaeleza kuwa Tudor alipitia kipindi kigumu binafsi baada ya kufiwa na baba yake hivi karibuni, jambo ambalo pia lilitambuliwa na klabu katika taarifa yao rasmi.

Hii ni mara ya pili kwa Spurs kubadili kocha ndani ya msimu huu wa 2025/26. Kabla ya Tudor, klabu hiyo ilimfuta kazi Thomas Frank mwezi Februari kutokana na matokeo mabaya pia.

Hadi sasa, Spurs hawajatangaza kocha mpya, lakini ripoti mbalimbali zinawataja Sean Dyche and Roberto De Zerbi kuwa kwenye uwezekano wa kurithi mikoba ya Tudor


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.