Kiungo mshambuliaji wa Chelsea FC, Cole Palmer, anaripotiwa kuanza kukata tamaa na maisha ndani ya klabu hiyo na huenda akatafuta kuondoka katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi.
Taarifa zinaeleza kuwa Palmer hajafurahishwa na mabadiliko ya mfumo wa uchezaji wa Chelsea, chini ya kocha wao Liam Rosenior, akiamini kuwa umemnyima nafasi na uhuru wa kuonyesha uwezo wake uwanjani. Aidha, anakosa kucheza pamoja na mshambuliaji Nicolas Jackson, ambaye alikuwa akisaidia kufungua nafasi kwa kunyoosha safu ya ulinzi wa wapinzani na kumpa Palmer uhuru wa kucheza.
Inaelezwa pia kuwa Palmer anatamani kurejea katika mji wake wa nyumbani, Manchester, ingawa Manchester United kwa sasa wanaweka kipaumbele katika kusajili wachezaji wa nafasi nyingine tofauti.
Wakati huo huo, mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wanaripotiwa kuonesha nia ya dhati ya kumsajili nyota huyo katika majira ya kiangazi, hatua inayoweza kuongeza ushindani mkubwa katika mbio za kuwania saini yake.
(Taarifa: Sun Sport)



