Klabu ya Tottenham Hotspur inatarajiwa kuanza mazungumzo rasmi na kocha Roberto De Zerbi kuhusu uwezekano wa kusaini mkataba wa miaka mitano kuinoa timu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Sky Sports, uongozi wa Tottenham umeweka wazi kuwa unahitaji suluhisho la kudumu kwenye nafasi ya ukocha kufuatia kuondoka kwa Igor Tudor, na si mpango wa muda mfupi.
Ripoti zinaeleza kuwa Spurs wanasukuma kwa nguvu kufanikisha dili hilo mapema iwezekanavyo, wakijaribu kupata idhini ya De Zerbi kuanza kazi mara moja, licha ya awali kumtazama kama chaguo la majira ya kiangazi.
Tottenham wanaamini De Zerbi ni kocha sahihi kwa mradi wao wa muda mrefu, na ndio sababu wameweka mezani ofa ya mkataba wa miaka mitano ili kumshawishi kukubali jukumu hilo haraka.



