Local,Normal News,Azam

Fei Toto na rekodi tamu misimu mitatu Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Mar 2026
Fei Toto na rekodi tamu misimu mitatu Azam Fc

Kiungo wa Azam FC, Feisal Salum maarufu kama 'Fei Toto', ameendelea kuwa nguzo muhimu ya timu hiyo baada ya kuonyesha kiwango cha juu katika misimu mitatu mfululizo ya Ligi Kuu Bara.

Msimu wa huu 2025–2026, Fei Toto ameshiriki moja kwa moja katika mabao 11, akifunga mabao sita na kutoa assisti tano. Bao lake dhidi ya Dodoma Jiji mnamo Machi 11, 2026, kwenye ushindi wa 3-0, limemfanya kuvunja rekodi ya mabao ya msimu uliopita aliyokuwa amefunga manne tu.

Msimu wa 2024–2025, Fei Toto aliongoza kwa assisti katika Ligi Kuu Bara baada ya kuisaidia Azam FC kufanikisha mabao 17 (mabao manne na assisti 13). Aidha, mwaka 2024 ulikuwa wa dhahabu kwa nyota huyu, baada ya kuisaidia timu yake kufanikisha mabao 27 (mabao 15 na assisti 12), akimzidi Stephane Aziz Ki wa Yanga aliyefanikisha mabao 21 (mabao 12 na assisti tisa).

Msimu wa 2023–2024, Fei Toto alifunga mabao 19 ya Ligi Kuu Bara, akishika nafasi ya pili kwa ufungaji miongoni mwa wachezaji, nyuma ya Aziz Ki aliyefunga 21. Pia, alijitokeza katika Kombe la Shirikisho (FA), akiisaidia Azam FC kufika fainali kwenye New Amaan Complex Juni 2, 2024, ambapo walipoteza kwa penalti 6-5 dhidi ya Yanga baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika 120.

Kwa misimu mitatu mfululizo, Fei Toto ameonyesha kuwa si tu mchezaji mwenye ubora wa kipekee, bali pia ni kiungo muhimu kinachochochea mafanikio ya Azam FC.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
48m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’