Siku nyingine, tetesi nyingine zenye uzito katika soka la Ulaya. Vilabu vikubwa vinaendelea kupanga mikakati ya majira ya joto huku baadhi ya majina makubwa yakihusishwa na uhamisho wa kushangaza. Hizi hapa ni habari kuu za leo:
Real Madrid wapanga mbadala wa Rodri
Real Madrid wanaendelea kuweka mipango ya kuimarisha kiungo wao, wakimlenga Rodri (29) kutoka Manchester City
Hata hivyo, iwapo dili hilo halitafanikiwa, watageukia Enzo Fernández (25) wa Chelsea au Adam Wharton (22) wa Crystal Palace.
Chanzo: Mundo Deportivo
Bei ya Rodri yafichuka
Ripoti zinaeleza kuwa itahitaji takriban pauni milioni 50 ili kuwashawishi Manchester City kumuuza Rodri.
Chanzo: Football Insider
Juventus wamfuatilia Manuel Ugarte
Juventus wanamchunguza kiungo wa Manchester United, Manuel Ugarte (24), kwa uwezekano wa kumsajili majira ya joto.
Chanzo: Gazzetta dello Sport
Newcastle wapata nafuu kuhusu Tonali
Newcastle United wamepata matumaini ya kumbakisha Sandro Tonali (25), licha ya kuvutiwa na vilabu vya Serie A.
Chanzo: Sportsport
Newcastle wakamilisha dili la kinda Johan Martinez
Newcastle United wamefikia makubaliano ya kumsajili chipukizi Johan Martinez (16) kutoka Independiente del Valle.
Chanzo: Fabrizio Romano
Nathan Ake arejea Chelsea?
Beki wa Manchester City, Nathan Aké (31), anaweza kurejea Chelsea, klabu yake ya zamani.
Chanzo: The Sun
Arsenal na Man United wamuwania Ferran Torres
Arsenal na Manchester United wanamtaka mshambuliaji wa Barcelona, Ferran Torres (26).
Chanzo: Fichajes
Chelsea na Liverpool wamuwania Lamine Camara
Chelsea na Liverpool wanaongoza mbio za kumsajili kiungo Lamine Camara (22) kutoka AS Monaco.
Chanzo: Ameotea
Bologna wamuwania Lorenzo Lucca
Bologna wanataka kumsajili mshambuliaji Lorenzo Lucca (25), ambaye yuko kwa mkopo Nottingham Forest kutoka Napoli.
Chanzo: Gazzetta dello Sport
Livramento aweza kuondoka Newcastle
Mazungumzo ya mkataba kati ya Newcastle United na Tino Livramento (23) yameripotiwa kukwama, hali inayoweza kufungua mlango wa kuondoka.
Chanzo: Football Insider
Liverpool vs Bayern kwa Lacroix
Liverpool wanakabiliwa na ushindani kutoka Bayern Munich katika mbio za kumsajili Maxence Lacroix (25) wa Crystal Palace.
Chanzo: TeamTalk
Barcelona wamuwania Julian Alvarez
Barcelona wamemuweka mshambuliaji wa Atlético Madrid, Julián Álvarez (26), kama lengo lao kuu la usajili majira ya joto.
Chanzo: Mundo Deportivo