Ndani ya Arsenal kunaongezeka hali ya kutoridhika kufuatia kuondolewa kwao kwenye FA Cup na Southampton, timu inayoshiriki EFL Championship.
Taarifa zinaeleza kuwa viongozi wa Arsenal wanaona ni jambo lisilokubalika kuondolewa na timu ya Championship, hali iliyozua presha kubwa ndani ya klabu hiyo.
Licha ya hali hiyo, uongozi bado unaamini kuwa Mikel Arteta ndiye mtu sahihi kuendeleza mradi wa muda mrefu wa timu. Hata hivyo, uvumilivu wao unaelezwa kufikia mwisho, wakihitaji kuona mafanikio ya haraka katika mfumo wa mataji.
Kwa sasa, matumaini ya Arsenal kubeba taji msimu huu yamebaki katika Premier League na UEFA Champions League pekee.
Inaelezwa wazi kuwa iwapo Arsenal watamaliza msimu huu bila kutwaa hata taji moja kati ya hayo mawili, basi huo unaweza kuwa mwisho wa Arteta ndani ya klabu hiyo, licha ya imani waliyoendelea kumuonyesha kwa muda mrefu.



