Kiungo chipukizi wa klabu ya PSG Mayulu amechagua rasmi kuichezea timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), nchi yenye asili ya wazazi wake.
Mazungumzo kati ya pande husika yamekamilika, huku taratibu za kumpatia passport ya kusafiria ya Congo zikiwa tayari zimeanza, hatua inayoonesha kujitoa kwake kwa dhati kuitumikia timu ya taifa ya DRC (the Leopards).
Huu ni uamuzi wenye uzito mkubwa na wa mfano, unaodhihirisha mapenzi yake kwa chimbuko lake pamoja na soka la Afrika kwa ujumla.
Mayulu sasa anaungana na kundi linalokua la wachezaji wenye uraia wa nchi mbili wanaochagua kwa fahari kuvaa rangi za DRC, wakiwa na dhamira ya kujenga mustakabali imara wa soka la Congo.



