Local,Normal News,Dodoma, Simba

Dodoma Jiji yajipanga kuikabili Simba kombe la CRDB

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Apr 2026
Dodoma Jiji yajipanga kuikabili Simba kombe la CRDB

Wakati presha ikizidi kupanda kuelekea mchezo wa hatua ya 16 bora ya Kombe la CRDB, kati ya Simba dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa Jumapili ya wiki hii, Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji Aman Josiah ameweka wazi dhamira yake ya kuiondosha Simba SC kwenye michuano hiyo.

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi Fountain Gate katika mchezo uliopita wa ligi kuu, Josiah amesema kikosi chake kina ari kubwa kuelekea mtanange huo uliopangwa kupigwa uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo jijini Dar es salaam.

Josiah amesema watakuwa na muda wa kuisoma Simba kimbinu na kufanya uchambuzi wa kina ili kuhakikisha wanaweka mikakati yao vyema.

Josiah alibainisha kuwa licha ya Simba kuwa na uzoefu mkubwa na historia nzuri kwenye mashindano hayo, hilo haliwatishi kwani watajipanga vyema.

β€œTunaiheshimu Simba, lakini hilo halimaanishi hatuna uwezo wa kushinda. Tunajipanga vizuri na kila mchezaji anatambua majukumu yake uwanjani,” alisema kocha huyo.

Mara ya mwisho Dodoma Jiji ilipokutana na Simba uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma katika mchezo wa ligi kuu, timu hizo zilitoka suluhu ya bila kufungana.

Mchezo wa April 12 ni wa mtoano kwa maana lazima mshindi apatikane ambaye atatinga robo fainali ya kombe la CRDB.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’