Local,Normal News,Yanga, Pamba, Singida, KMC

Yanga ugenini Mwanza, Singida BS nyumbani dhidi ya KMC

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Apr 2026
Yanga ugenini Mwanza, Singida BS nyumbani dhidi ya KMC

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo raundi ya 18 ambapo mechi mbili zinatarajiwa kupigwa mkoani Singida na Mwanza.

Singida BS inayopitia misukosuko baada ya mfululizo wa matokeo mabaya, itakuwa nyumbani uwanja wa Airtel kuikaribisha KMC ambayo pia inachungulia shimo la kuteremka daraja.

Juzi Singid BS ilitangaza kulifuta benchi la ufundi pamoja kuwakata wachezaji wote mishahara kwa asilimia 40 kufuatia mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha.

Timu zote zinakutana zikiwa zimetoka kutimua makocha hali inayofanya mchezo huo kuwa muhimu kwa kila ili kupunguza presha inazozikabili timu hizo.

Mtanange kati ya Singida BS dhidi ya KMC unatarajiwa kupigwa saa 8 mchana na kufuatiwa na mchezo kati ya Pamba Jiji dhidi ya Yanga.

Hii ni mechi nyingine inayotarajiwa kuwa na upinzani mkali hasa kutokana na rekodi zinazokutana.

Pamba Jiji hawajapoteza mchezo uwanja wa nyumbani, leo watakuwa na kazi ngumu ya kuwazuia Wananchi kuondoka na alama tatu.

Yanga wakiwa vinara wa ligi, wanazihitaji alama zote tatu ili kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi ambao mpaka sasa wanaongoza kwa tofauti ya alama 6.

Yanga ilitua Mwanza juzi ambapo jana vijana wa kocha Pedro Goncalves wakafanya maandalizi yao ya mwisho katika uwanja wa CCM Kirumba.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’