Local,Normal News,Simba, Singida

Sowah na Simba mwisho umefika

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Apr 2026
Sowah na Simba mwisho umefika

Mshambuliaji wa Simba SC Jonathan Sowah, amewasilisha barua rasmi kwa uongozi wa klabu hiyo akiomba kuvunja mkataba wake, kufuatia mgogoro wa kinidhamu unaomkabili.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa hatua hiyo imekuja baada ya mchezaji huyo kusimamishwa na klabu kutokana na tuhuma za utovu wa nidhamu. Awali, Sowah alipewa nafasi ya kujitetea huku uongozi ukisubiri kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu hatma yake.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Sowah ambaye amefunga mabao matatu msimu huu, anapinga tuhuma zinazomkabili na amependekeza mkataba wake uvunjwe kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba, imethibitisha kuwa tayari mchezaji huyo amechukua hatua rasmi kutaka kuachana na klabu hiyo.

Inaelezwa kuwa hata kabla ya ombi hilo, uongozi wa Simba ulikuwa unaelekea kwenye uamuzi wa kutomrejesha mchezaji huyo kikosini kutokana na mwenendo wake wa kinidhamu.

Sowah alijiunga na Simba akitokea Ghana akiwa na matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki, lakini changamoto za nidhamu zimeonekana kuathiri safari yake ndani ya kikosi hicho.

Hadi sasa, uongozi wa Simba haujatoa tamko rasmi kuhusu hatma ya mchezaji huyo, lakini ni wazi Sowah hatarajiwi kuendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Simba.

More Stories

Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
27m ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
28m ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
1h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
2h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
9h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
14h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
14h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
16h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
16h ago
READ MORE β†’