Local,Transfer News,Yanga, Azam

Yanga kuizidi ujanja Azam Fc kwa Akaminko?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Apr 2026
Yanga kuizidi ujanja Azam Fc kwa Akaminko?

Klabu ya Yanga SC ya Dar es Salaam inaripotiwa kuanza mchakato wa kumnasa kiungo mkabaji wa Azam FC raia wa Ghana, James Akaminko, ambaye mkataba wake na klabu hiyo unaelekea ukingoni.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya tasnia ya usajili, Yanga imeanza mazungumzo ya awali ikiwa na lengo la kumsajili kiungo huyo mwenye uzoefu mkubwa katika Ligi Kuu Tanzania Bara, katika harakati za kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao.

Hii si mara ya kwanza kwa Yanga kuonyesha nia ya kumsajili Akaminko, ambapo awali klabu hiyo iliwahi kujaribu kumjumuisha katika mazungumzo ya usajili wakati wa mchakato wa uhamisho wa mchezaji Feisal Salum kwenda Azam FC, pamoja na jina la Kipre Junior ambaye kwa sasa anacheza MC Alger ya Algeria.

Kwa kipindi hicho, Azam FC ilifanikiwa kumbakiza kiungo huyo ambaye ameitumikia klabu hiyo kwa misimu minne, akiwa miongoni mwa wachezaji muhimu katika safu ya kiungo.

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa hali ya sasa inaweza kuwa tofauti, kutokana na mchezaji huyo mwenyewe kuonyesha nia ya kutafuta changamoto mpya baada ya muda mrefu akiwa Azam FC, jambo linaloweza kufungua milango ya uhamisho wake.

Iwapo Yanga SC itafanikiwa kukamilisha dili hilo, huenda ikawa na mabadiliko katika safu yake ya kiungo, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuachana na Moussa Balla Conte ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo katika klabu ya Raja Casablanca ya Morocco.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’