International,Normal News,Barcelona, Atletico madrid, UEFA

Barcelona waiomba Uefa kukagua uwanja metropolitano

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
14 Apr 2026
Barcelona waiomba Uefa kukagua uwanja metropolitano

Klabu ya FC Barcelona imewasilisha ombi rasmi kwa UEFA ikiitaka ifanye ukaguzi wa uwanja wa Estadio Metropolitano, unaotumiwa na Atlético Madrid, kufuatia wasiwasi kuhusu hali ya nyasi.

Kwa mujibu wa Barcelona, nyasi za uwanjani humo zinadaiwa kuwa ndefu kupita kiwango kinachokubalika, hali ambayo inaweza kuathiri mtindo wao wa kucheza mpira wa pasi za chini. Klabu hiyo imesisitiza kuwa UEFA ndiyo mamlaka yenye jukumu la kuhakikisha kunakuwepo usawa na haki kwa pande zote, hivyo kuomba hatua zichukuliwe mapema kabla ya mchezo husika.

Hata hivyo, Atlético Madrid wamekanusha madai hayo wakieleza kuwa uwanja uko katika hali ya kawaida na hauhitaji ukaguzi wowote wa ziada. Wenyeji hao wamesisitiza kuwa nyasi ipo katika kiwango kinachotumika mara kwa mara bila tatizo lolote.

Kwa sasa, uamuzi wa mwisho uko mikononi mwa UEFA, ambao wanatarajiwa kuamua iwapo watafanya ukaguzi rasmi au watakataa ombi hilo. Sakata hili limeongeza mvutano kuelekea mechi hiyo muhimu, huku pande zote zikiendelea kusimamia misimamo yao.

Chanzo; @Marca

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
6h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
11h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
11h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
13h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
14h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
17h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
19h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
20h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’