Klabu ya Simba SC inaripotiwa kuanza mchakato wa kuwania saini ya kiungo mshambuliaji wa Medeama SC Salim Adams, kufuatia msimu wake mzuri katika Ligi Kuu ya Ghana.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 ameendelea kung’ara akiwa miongoni mwa wachezaji muhimu wa Medeama SC msimu huu, kutokana na mchango wake mkubwa katikati ya uwanja na eneo la ushambuliaji.





