Klabu ya Young Africans SC imeendeleza ubabe wake katika Ligi Kuu ya NBC baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 6-0 dhidi ya Mbeya City FC katika mchezo uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.
Katika mchezo huo, Yanga walionyesha kiwango cha juu tangu mwanzo hadi mwisho, wakimaliza kazi mapema kwa kufunga mabao matano ndani ya kipindi cha kwanza.





