International,Normal News,Zamalek, Belouizdad

Zamalek yatangulia fainali kombe la Shirikisho la CAF

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Apr 2026
Zamalek yatangulia fainali kombe la Shirikisho la CAF

Klabu ya Zamalek SC imefanikiwa kutinga fainali ya CAF Confederation Cup baada ya kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya CR Belouizdad katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali.

Mchezo huo uliochezwa Ijumaa jijini Cairo uliwakutanisha wababe hao wa Afrika Kaskazini, huku Zamalek wakitumia vyema ushindi wao wa awali wa bao 1-0 walioupata ugenini nchini Algeria, matokeo yaliyowapa faida ya jumla ya mabao 1-0.

Katika pambano hilo la marudiano, timu zote zilicheza kwa tahadhari kubwa, zikilenga kuepuka makosa. CR Belouizdad walihitaji ushindi ili kusonga mbele, lakini walishindwa kupenya safu imara ya ulinzi ya Zamalek iliyokuwa makini kwa dakika zote 90.

Matokeo hayo yanawapeleka Zamalek katika hatua ya fainali ya michuano hiyo, wakitarajia kupambana na mshindi wa nusu fainali nyingine kati OC Safi dhidi ya USM Alger. Mafanikio hayo yanaendeleza rekodi nzuri ya klabu hiyo katika mashindano ya vilabu barani Afrika.

Kwa upande wa CR Belouizdad, ndoto yao ya kufika fainali imeishia hatua ya nusu fainali licha ya kuonyesha ushindani mkubwa katika michezo yote miwili.

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’