International,Normal News,Sundowns, Esperance, Local

Sundowns yatangulia fainali ligi ya mabingwa baada ya ushindi dhidi ya Esperance

Joel JJ By Joel JJ
18 Apr 2026
Sundowns yatangulia fainali ligi ya mabingwa baada ya ushindi dhidi ya Esperance

Klabu ya Mamelodi Sundowns imefanikiwa kutinga fainali ya CAF Champions League 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Espérance Sportive de Tunis katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali uliopigwa katika Uwanja wa Loftus Versfeld Stadium.

Ushindi huo umeifanya Sundowns kufuzu kwa jumla ya mabao 2-0, kufuatia ushindi wa 1-0 walioupata ugenini nchini Tunisia katika mchezo wa kwanza uliochezwa Aprili 12, 2026.

Bao pekee la mchezo wa leo lilifungwa na mshambuliaji Brayan León, aliyefunga kwa kufuatilia mpira wa kurejea baada ya penalti yake kuokolewa na kipa wa Esperance.

Katika mchezo huo, Sundowns walionyesha nidhamu ya hali ya juu wakitumia vyema nafasi zao chache za kufunga huku wakijipanga imara katika safu ya ulinzi kuzuia mashambulizi ya wapinzani wao.

Licha ya Esperance kuongeza presha hasa katika kipindi cha pili, walishindwa kupata bao kutokana na ukosefu wa umakini katika umaliziaji.

Kwa matokeo hayo, Sundowns wamefanikiwa kufika fainali ya mashindano hayo kwa mara ya tano katika historia yao, baada ya kufika hatua hiyo mwaka 2001, 2016, 2024, 2025 na sasa 2026.

Katika hatua ya fainali, Sundowns watakutana na mshindi kati ya klabu za Morocco, RSB Berkane na AS FAR Rabat, katika michezo miwili itakayochezwa Mei 15 na Mei 24, 2026.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE →
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
7h ago
READ MORE →
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE →
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE →
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE →
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE →
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE →
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE →
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE →
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE →