Michuano ya kombe la Muungano inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Jumanne, April 21 ratiba ya michuano hiyo ikiwekwa hadharani leo.
Mabingwa watetezi wa michuano hiyo Yanga watashuka dimbani Jumanne kumenyana na M/Makumbi mchezo utakaopigwa saa 1:15 usiku.
Kama Yanga itatinga nusu fainali, katika hatua hiyo itakutana na mshindi wa mchezo kati ya KVZ dhidi ya Azam Fc.





