Local,Normal News,Yanga

Yanga yawasili Zanzibar tayari kwa kombe la Muungano

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Apr 2026
Yanga yawasili Zanzibar tayari kwa kombe la Muungano

Kikosi cha Yanga kimewasili Visiwani Zanzibar leo tayari kushiriki michuano ya kombe la Muungano inayotarajiwa kuanza kesho Jumanne, April 21 katika uwanja wa New Amaan Compex.

Yanga itafungua pazia ya michuano hiyo hapo kesho kwa mchezo dhidi ya Muembe Makumbi utakaopigwa saa 1 usiku dimba la Amaan.

Yanga ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo wakitwaa yaji msimu uliopita ikiwa huu ni msimu wa tatu tangu michuano hiyo iliporejeshwa rasmi.

Msimu wa kwanza Simba waliibuka mabingwa, msimu huu klabu nane zikichuana kuwania taji hilo.

Bingwa wa michuano hiyo mwaka huu ataondoka na kitita cha Shilingi Milioni 150, ikiwa ni ongezeko la mara tatu zaidi ya zawadi ya mwaka jana (Milioni 50). Mshindi wa pili atajinyakulia Shilingi Milioni 100.

Klabu za Yanga, Simba, Azam Fc na Singida BS zitashiriki michuano hiyo zikiwakilisha Tanzania bara wakati KVZ, Mlandege, Mafunzo na Muembe Makumbi zikiwakilisha upande wa Zanzibar

More Stories

Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
4h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
4h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
6h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
7h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
10h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
12h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
13h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
Kocha Dimitar Pantev ateuliwa kuwa kocha mpya wa Richard Bay.
1d ago
READ MORE β†’