Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube anachuana vikali na mshambuliaji wa Namungo Fc Fabrice Ngoy wote wakifunga mabao nane kwenye ligi kuu ya NBC msimu huu.
Wakati Yanga ikiichapa Mbeya City mabao 6-0, Dube alifunga mabao mawili na hivyo kumfikia Ngoy ambaye amesimama kwenye mabao nane kwa muda mrefu.






