Local,Normal News,Yanga, Namungo

Dube, Ngoy wachuana ufungaji bora ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2026
Dube, Ngoy wachuana ufungaji bora ligi kuu

Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube anachuana vikali na mshambuliaji wa Namungo Fc Fabrice Ngoy wote wakifunga mabao nane kwenye ligi kuu ya NBC msimu huu.

Wakati Yanga ikiichapa Mbeya City mabao 6-0, Dube alifunga mabao mawili na hivyo kumfikia Ngoy ambaye amesimama kwenye mabao nane kwa muda mrefu.

Aidha nyota wengine wa Yanga Mudathir Yahya na Pacome Zouzoua nao wako karibu na vinara hao wa mabao kila mmoja akifunga mabao 7.

Kiungo mshambuliaji wa Azam Fc Feisal Salum 'Fei Toto' nae ameweka kambani mabao saba pia akiwa kinara wa kutoa pasi za mabao ambapo anazo 7.

Feisal anaungana na nyota mwingine wa Azam Fc, winga Idd Nado ambaye pia amepachika mabao 7.

Katika orodha hiyo ya mabao 7 pia yumo kiungo mshambuliaji wa JKT Tanzania, Saleh karabaka anayeitumikia timu hiyo kwa mkopo akitokea klabu ya Simba.

Washambuliaji Laurindo Aurelio 'Depu' wa Yanga na Suleiman Mwalimu wa Simba wao wamepachika mabao 6 kila mmoja.

More Stories

Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
3h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
8h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
8h ago
READ MORE β†’
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
Nyota Stars waingia kambini tayari kwa mechi za kufuzu Afcon 2027
10h ago
READ MORE β†’
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
Simba kujichimbia Afrika Kusini kujiandaa na Kariakoo Derby
10h ago
READ MORE β†’
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
Madrid Derby: Atletico na Real kwenye vita ya majirani
14h ago
READ MORE β†’
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
Hii hapa rekodi tamu ya Barker Ligi Kuu
16h ago
READ MORE β†’
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
Sundowns kuchuana na Al Ahli katika vita ya Afrika na Asia
17h ago
READ MORE β†’
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
Ft: Yanga 1-0 St George, Yanga yapata ushindi mechi ya kirafiki.
1d ago
READ MORE β†’
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
Dockers Derby yarudi baada ya miaka 14, Ulinzi wa London ukiimarishwa.
1d ago
READ MORE β†’