Klabu ya FC Barcelona imepiga hatua kubwa kuelekea kutwaa ubingwa wa La Liga baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Celta Vigo katika mchezo uliopigwa Jumatano usiku, April 22, 2026.
Bao pekee la ushindi lilifungwa na kinda nyota Lamine Yamal dakika ya 38 kwa njia ya penalti, baada ya yeye mwenyewe kuchezewa madhambi ndani ya eneo la hatari.





