International,Normal News,World Cup, Local

Italia yapigiwa chapuo ichukue nafasi ya Irani kombe la Dunia 2026

Joel JJ By Joel JJ
23 Apr 2026
Italia yapigiwa chapuo ichukue nafasi ya Irani kombe la Dunia 2026

Pendekezo la kuitaka FIFA kuiondoa Iran na nafasi yake kuchukuliwa na Italia katika fainali za FIFA World Cup 2026 limezua mjadala mkubwa katika ulimwengu wa soka na siasa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na gazeti la Financial Times, Paolo Zampolli, mjumbe wa Donald Trump, amethibitisha kuwasilisha pendekezo hilo kwa Rais huyo wa Marekani pamoja na Rais wa FIFA, Gianni Infantino.

“Nimependekeza kwa Trump na Infantino kuwa Italy ichukue nafasi ya Iran. Ni ndoto kuona Azzurri ikicheza Kombe la Dunia linalofanyika Marekani,” alinukuliwa Paolo Zampolli akieleza, akisisitiza historia ya Italia yenye mataji manne ya dunia.

Taarifa zinaeleza kuwa mpango huo unahusishwa pia na juhudi za kurekebisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Donald Trump na Waziri Mkuu wa Italia, Giorgia Meloni.

Inaelezwa kuwa uhusiano huo uliwahi kuzorota kufuatia kauli za Trump katika muktadha wa mvutano wa kimataifa unaohusisha Iran, hali iliyochochea mjadala wa kisiasa kuingia katika masuala ya michezo.

Hakuna uamuzi rasmi FIFA

Pamoja na mjadala huo, FIFA haijatoa tamko lolote rasmi la kuiondoa Iran kwenye mashindano hayo.

Iran tayari imefuzu kushiriki FIFA World Cup 2026 kupitia michuano ya kufuzu ya bara la Asia na inaendelea na maandalizi kama kawaida kuelekea fainali hizo zitakazofanyika Marekani, Canada na Mexico.

Kwa upande wa Italia, timu hiyo ilishindwa kufuzu baada ya kupoteza kwa mikwaju ya penalti 4-1 dhidi ya Bosnia and Herzegovina katika hatua ya mchujo wa Ulaya, hivyo kubaki nje ya mashindano hayo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →