Yamal amemaliza msimu Barcelona

Joel JJ By Joel JJ • 23rd April 2026


Yamal amemaliza msimu Barcelona

Klabu ya FC Barcelona imethibitisha kuwa nyota wake kijana, Lamine Yamal (18), atakosa mechi zote zilizosalia za msimu huu baada ya kupata jeraha la misuli ya mguu wa kushoto.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu hiyo, vipimo vya kitabibu vilivyofanyika baada ya mchezo wa La Liga dhidi ya Celta Vigo vilibaini kuwa Yamal amepata jeraha katika misuli ya biceps femoris, sehemu ya nyuma ya paja la mguu wa kushoto.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mchezaji huyo atalazimika kupumzika kikamilifu ili kupona, hatua inayomaanisha hatoshiriki tena katika mechi yoyote ya msimu huu wa 2025/2026.

Kutokuwepo kwa Yamal ni pigo kwa FC Barcelona katika kipindi muhimu cha mwisho wa msimu, ambapo klabu hiyo inakaribia kutwaa ubingwa wa La Liga ikihitaji kushinda michezo angalau michezo mitatu kati ya sita iliyosalia.

Yamal amekuwa miongoni mwa wachezaji muhimu wa kikosi hicho msimu huu, akichangia mabao na pasi za mwisho katika mechi kadhaa muhimu, huku akionekana kuwa moja ya vipaji vikubwa vinavyoibukia Ulaya.

Licha ya majeraha hayo, taarifa zinaeleza kuwa matarajio ya klabu na timu ya taifa ni kuona Yamal akirejea akiwa fiti kabisa kwa ajili ya majukumu ya kimataifa na timu ya taifa ya Hispania.

Mchezaji huyo anatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Spain kitakachoshiriki katika maandalizi na hatimaye fainali za FIFA World Cup 2026 zitakazofanyika Marekani, Canada na Mexico.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE →
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE →
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE →
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE →
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE →
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE →
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE →
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE →
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE →
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE →