International,Normal News,Barcelona

Yamal amemaliza msimu Barcelona

Joel JJ By Joel JJ
23 Apr 2026
Yamal amemaliza msimu Barcelona

Klabu ya FC Barcelona imethibitisha kuwa nyota wake kijana, Lamine Yamal (18), atakosa mechi zote zilizosalia za msimu huu baada ya kupata jeraha la misuli ya mguu wa kushoto.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya klabu hiyo, vipimo vya kitabibu vilivyofanyika baada ya mchezo wa La Liga dhidi ya Celta Vigo vilibaini kuwa Yamal amepata jeraha katika misuli ya biceps femoris, sehemu ya nyuma ya paja la mguu wa kushoto.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mchezaji huyo atalazimika kupumzika kikamilifu ili kupona, hatua inayomaanisha hatoshiriki tena katika mechi yoyote ya msimu huu wa 2025/2026.

Kutokuwepo kwa Yamal ni pigo kwa FC Barcelona katika kipindi muhimu cha mwisho wa msimu, ambapo klabu hiyo inakaribia kutwaa ubingwa wa La Liga ikihitaji kushinda michezo angalau michezo mitatu kati ya sita iliyosalia.

Yamal amekuwa miongoni mwa wachezaji muhimu wa kikosi hicho msimu huu, akichangia mabao na pasi za mwisho katika mechi kadhaa muhimu, huku akionekana kuwa moja ya vipaji vikubwa vinavyoibukia Ulaya.

Licha ya majeraha hayo, taarifa zinaeleza kuwa matarajio ya klabu na timu ya taifa ni kuona Yamal akirejea akiwa fiti kabisa kwa ajili ya majukumu ya kimataifa na timu ya taifa ya Hispania.

Mchezaji huyo anatarajiwa kuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Spain kitakachoshiriki katika maandalizi na hatimaye fainali za FIFA World Cup 2026 zitakazofanyika Marekani, Canada na Mexico.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →