International,Normal News,Manchester United, Brentford

Manchester United yajiimarisha kufuzu ligi ya mabingwa Ulaya

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Apr 2026
Manchester United yajiimarisha kufuzu ligi ya mabingwa Ulaya

Klabu ya Manchester United imeongeza matumaini ya kumaliza katika nafasi za juu za Premier League baada ya ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Brentfordkatika mchezo uliopigwa Old Trafford Jumatatu usiku.

Ushindi huo umeifanya Manchester United kujiimarisha katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi, alama tatu mbele ya Liverpool hatua inayowaweka karibu zaidi kufuzu kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

Mabao ya mapema yaamua mchezo

Katika mchezo huo, United walianza kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza mapema kupitia kiungo mkongwe Casemiro, aliyefunga kwa kichwa dakika ya 11 kufuatia mpira wa kona.

Shinikizo liliendelea na kabla ya mapumziko mshambuliaji Benjamin Sesko aliongeza bao la pili dakika ya 37, akimalizia shambulizi la kushtukiza lililoanzishwa na nahodha Bruno Fernandes.

Brentford walijaribu kurejea mchezoni kipindi cha pili, lakini walifanikiwa kupata bao moja tu kupitia Mathias Jensen mwishoni mwa mchezo, huku United wakidhibiti ushindi huo hadi mwisho.

Matokeo hayo yameifanya Manchester United kufikisha pointi 61 na kubaki nafasi ya tatu, wakiwa mbele kwa pointi 11 dhidi ya nafasi ya sita huku michezo michache ikisalia.

Ushindi huo unawaweka katika nafasi nzuri sana ya kufuzu Ligi ya Mabingwa, huku ushindani wa nafasi nne za juu ukiendelea kupamba moto.

Kocha atoa tahadhari

Kocha wa muda Michael Carrick amesisitiza kuwa licha ya ushindi huo muhimu, bado timu inapaswa kuendelea kupambana hadi mwisho wa msimu.

Amesema mafanikio ya kufuzu michuano ya Ulaya hayapaswi kuwafanya wachezaji kuridhika mapema, akihimiza nidhamu na juhudi kuendelea katika mechi zilizosalia.

More Stories

Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
3h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
5h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
7h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
7h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
9h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
9h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
17h ago
READ MORE β†’
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
Mamelodi Sundowns yaibuka kidedea mbele ya Al Ahli
21h ago
READ MORE β†’
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
Arsenal yaduwazwa 3-0 na Brighton
21h ago
READ MORE β†’