Local,Normal News,Simba, Yanga

Simba yaunguruma Zanzibar, yatwaa ubingwa Muungano Cup baada ya ushindi dhidi ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Apr 2026
Simba yaunguruma Zanzibar, yatwaa ubingwa Muungano Cup baada ya ushindi dhidi ya Yanga

Hatimaye mambo yamebadilika! Simba SC wametwaa ubingwa wa Kombe la Muungano baada ya ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya watani wao wa jadi Yanga SC katika fainali kali iliyochezwa kwenye New Amaan Complex.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa kwa dakika zote 120, huku timu zote zikionesha ari, nidhamu na mbinu za hali ya juu. Dakika 90 za kawaida zilimalizika kwa suluhu ya bila kufungana, na hata katika muda wa nyongeza mambo yaliendelea kuwa magumu huku kila upande ukisaka bao la ushindi.

Dakika za mwisho kabisa ndipo drama ilipojitokeza. Kiungo mshambuliaji Clatous Chama alifanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari na Edmund John, hali iliyomlazimu mwamuzi kuamuru ipigwe penati. Bila presha, Suleiman Mwalimu aliitumia vyema nafasi hiyo na kufunga bao pekee lililoipa Simba ushindi huo muhimu.

Ulikuwa ushindi uliopatikana kwa jasho na kujituma kwa kiwango cha juu kutoka kwa wachezaji wa Simba, ambao walidhibiti mchezo kwa nidhamu na kupambana hadi dakika ya mwisho. Huu pia ni ushindi unaovunja matarajio ya Yanga waliokuwa na mwendelezo mzuri wa matokeo katika mechi za hivi karibuni.

Kocha Steve Barker pamoja na benchi lake la ufundi wanastahili pongezi kwa mbinu zilizowezesha timu yao kufikia mafanikio haya. Ushindi huu unaashiria mwanzo wa enzi mpya kwa Simba, huku mashabiki wakianza kuamini tena katika ubora wa timu yao.

Katika michuano hiyo pia Simba imechukua tuzo za kipa bora Hussein Abel, Hussein Mbegu akibeba tuzo ya mchezaji bora chipukizi, Rushine de Reuck akibabe tuzo ya mchezaji bora wa mashindano huku Seleman Mwalimu akichukua tuzo ya mfungaji bora wakati kocha bora ni Steve Barker

Kwa kutwaa ubingwa huo, Simba pia imeondoka na kitita cha Tsh Milioni 150 huku Yanga iliyomaliza nafasi ya pili ikiondoka na kitita cha Tsh Milioni 100.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’