Simba yamtaka beki Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st May 2026


Simba yamtaka beki Azam Fc

Klabu ya Simba SC imeanza rasmi mazungumzo na mlinzi wa kulia wa Azam FC Nathaniel Chilambo, katika harakati za kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani, Simba imeweka mkazo kwenye eneo la ulinzi wa pembeni, hasa upande wa kulia, ambako kwa sasa kuna nahodha Shomari Kapombe pamoja na David Kameta.

Hata hivyo, Kameta bado hajafanikiwa kumpa ushindani wa moja kwa moja Kapombe, jambo lililoifanya benchi la ufundi kuona kuna haja ya kuimarisha eneo hilo.

Kocha wa Simba, Steve Barker, ameripotiwa kupendekeza maboresho ya eneo hilo, akitaka timu iwe na chaguo zaidi katika nafasi muhimu za ulinzi.

Inaelezwa kuwa mkataba wa Chilambo na Azam FC unafikia tamati mwishoni mwa msimu huu, hali inayomruhusu mchezaji huyo kuingia kwenye mazungumzo na klabu yoyote inayomuhitaji. Hii imeifanya Simba kuchukua hatua za mapema ili kumnasa beki huyo kabla ya dirisha rasmi la usajili kufunguliwa.

Vyanzo vinaeleza kuwa uongozi wa Simba tayari umeandaa ofa ya mkataba wa miaka miwili, ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuimarisha kikosi. Endapo makubaliano yatakamilika, Chilambo atasaini mkataba wa awali (pre-contract) kabla ya kujiunga rasmi.

Simba SC pia imeonyesha kubadilisha mkakati wake wa usajili, ambapo sasa inahakikisha inakamilisha mazungumzo mapema kabla ya dirisha la uhamisho kufunguliwa, ili kuepuka ushindani mkali wa soko.


  

More Stories

Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Azam Fc hiyooo fainali, yaichapa Yanga 3-2 nusu fainali
Today, READ MORE β†’
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Azam Fc 3-2 Yanga, CRDB Cup
Today, READ MORE β†’
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Ni Azam Fc vs Yanga, nani anakwenda fainali kombe la CRDB?
Today, READ MORE β†’
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Liverpool kuongeza dau kumnasa Diomande
Today, READ MORE β†’
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Prisons wamefufua matumaini kusalia ligi kuu
Today, READ MORE β†’
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Tunisia yaaga kombe la Dunia kwa aibu, yapigwa 4-0 na Japan
Today, READ MORE β†’
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Ivory Coast yapoteza dhidi ya Ujerumani dakika za jioni
Today, READ MORE β†’
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Real Madrid yakana kuwasiliana na Olise, wakala wake
Yesterday, READ MORE β†’
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Simba 4-0 Coastal Union, CRDB Cup
Yesterday, READ MORE β†’
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Simba yaifumua Coastal Union 4-0, yatinga fainali ya CRDB Bank Cup
Yesterday, READ MORE β†’