Local,Transfer News,Simba, Azam

Simba yamtaka beki Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 May 2026
Simba yamtaka beki Azam Fc

Klabu ya Simba SC imeanza rasmi mazungumzo na mlinzi wa kulia wa Azam FC Nathaniel Chilambo, katika harakati za kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani, Simba imeweka mkazo kwenye eneo la ulinzi wa pembeni, hasa upande wa kulia, ambako kwa sasa kuna nahodha Shomari Kapombe pamoja na David Kameta.

Hata hivyo, Kameta bado hajafanikiwa kumpa ushindani wa moja kwa moja Kapombe, jambo lililoifanya benchi la ufundi kuona kuna haja ya kuimarisha eneo hilo.

Kocha wa Simba, Steve Barker, ameripotiwa kupendekeza maboresho ya eneo hilo, akitaka timu iwe na chaguo zaidi katika nafasi muhimu za ulinzi.

Inaelezwa kuwa mkataba wa Chilambo na Azam FC unafikia tamati mwishoni mwa msimu huu, hali inayomruhusu mchezaji huyo kuingia kwenye mazungumzo na klabu yoyote inayomuhitaji. Hii imeifanya Simba kuchukua hatua za mapema ili kumnasa beki huyo kabla ya dirisha rasmi la usajili kufunguliwa.

Vyanzo vinaeleza kuwa uongozi wa Simba tayari umeandaa ofa ya mkataba wa miaka miwili, ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kuimarisha kikosi. Endapo makubaliano yatakamilika, Chilambo atasaini mkataba wa awali (pre-contract) kabla ya kujiunga rasmi.

Simba SC pia imeonyesha kubadilisha mkakati wake wa usajili, ambapo sasa inahakikisha inakamilisha mazungumzo mapema kabla ya dirisha la uhamisho kufunguliwa, ili kuepuka ushindani mkali wa soko.

More Stories

Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
Manchester City yaichapa Sunderland 5–3 katika mechi ya mabao nane
52m ago
READ MORE β†’
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
Atletico yang’ara kwenye dabi, Real Madrid aangukia pua ugenini
1h ago
READ MORE β†’
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
Nyota Geita Gold afunguka rafu ya Aziz KI, Ilikuwa bahati mbaya
7h ago
READ MORE β†’
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
LAPORTA: Atletico kumuuza Alvarez kwa timu yeyote isipokuwa Barcelona
9h ago
READ MORE β†’
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
Ngorongoro Heroes yatangulia nusu fainali CECAFA U20 kwa kishindo
11h ago
READ MORE β†’
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
Samatta afunga bao lake la pili, Le Havre ikipoteza
11h ago
READ MORE β†’
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
Salah hakamatiki Uturuki, apiga hat-trik Trabzonspor ikiifumua Galatasaray 4-0
11h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
Azam Fc yaonywa, Yanga yakumbana na faini - Kamati ya saa 72
12h ago
READ MORE β†’
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
Mshambuliaji wa zamani Yanga aibukia Zambia
12h ago
READ MORE β†’
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
Barcelona yaendeleza kichapo Laliga ikimfunga Sevilla, Raphinha hashikiki.
20h ago
READ MORE β†’