Timu ya TRA United imeendeleza kasi yake katika Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Katika mchezo huo, TRA United ilionyesha ubora mkubwa tangu dakika za mwanzo hadi mwisho, ikiutumia vyema uwanja wa ugenini kuondoka na alama zote tatu muhimu.





